UgaidiSomalia
Somalia na Marekani wawashambulia wapiganaji wa al-Shabaab
18 Aprili 2025Matangazo
Mashambulizi hayo yalifanywa katika mji wa Adan Yabaal, takriban kilomita 220 kaskazini mwa mji mkuu Mogadishu wakati wapiganaji wa Al-Shabaab walipovamia mji huo muhimu wenye kambi ya makamanda wa kijeshi wa Somalia. Mashambulizi mengine yaliwaua wapiganaji 35 katika mji wa kusini magharibi wa Baidoi.
Kuongezeka kwa mashambulizi ya al-Shabaab yenye mafungamano na kundi la kigaidi la Al-Qaeda, ikiwa ni pamoja na mashambulizi dhidi ya msafara wa Rais Hassan Sheikh Mohamud , yamekuwa yakizidisha wasiwasi wa kuibuka tena kwa makundi hayo ya itikadi kali.