MigogoroAfrika
MSF yalaani shambulio dhidi ya hospitali Goma
12 Aprili 2025Matangazo
Taarifa ya MSF iliyotolewa Ijumaa imeeleza kuwa kundi la wanaume 20 wenye silaha lilivamia eneo la hospitali hiyo na kuwatafuta watu waliojificha hospitalini.
Ripoti hiyo imeongeza kuwa wafanyakazi wawili wa hospitali ya Kyeshero walipigwa vibaya na kuwa pamoja na kwamba wavamizi hawakuingia ndani ya hospitali, risasi zilipenya ndani ya baadhi ya vyumba vya wagonjwa.
Soma zaidi: MSF yawataka wapiganaji Kongo kutozishambulia hospitali na raia
Mtu mmoja alijeuwawa na watu wengine watatatu walijeruhiwa katika mkasa huo. Mratibu wa masuala ya dharura wa MSF Margot Grelet, kwa Goma na Kivu Kaskazini amesema matukio ya aina hiyo hayakubaliki na kamwe hayapaswi kujirudia.