Shambulizi la Urusi lawauwa watu 18 nchini Ukraine
5 Aprili 2025Katika ujumbe kupitia mtandao wa kijamii wa Telegram, gavana wa eneo la Dnipropetrovsk, Sergiy Lysak, amesema leo kuwa watu 61 pia wamejeruhiwa na kwamba operesheni ya uokozi ilimalizika usiku.
Lysak amesema watoto 12 walijeruhiwa katika shambulizihilo la Ijumaa na kuongeza kuwa huo ni uchungu ambao mtu hawezi hata kumtakia adui yake.
Shambulizi lililenga makaazi ya watu karibu na uwanja wa michezo wa watoto
Mkuu wa utawala wa kijeshi katika eneo hilo la Kryvyi, Rih Oleksandr Vilkul, amesema kombora hilo lilipiga eneo la makaazi ya watu karibu na uwanja wa michezo wa watoto hapo jana.
Urusi yasema imeshambulia mgahawa mmoja Kryvyi Rih
Wizara ya ulinzi ya Urusi imesema kuwa jeshi lake limeshambulia mgahawa mmoja katika mji huo ambapo makamanda wa vikosi na wakufunzi wa mataifa ya Magharibi walikuwa wanakutana.
Wizara hiyo imeongeza kuwa vikosi vya jeshi lake la ulinzi wa anga, vimedungua na kuharibu droni 49 za Ukraine usiku kucha.