Shambulizi la Israel Gaza lasababisha mauaji ya watu 52
26 Mei 2025Matangazo
Msemaji wa taasisi ya ulinzi wa raia Mahmud Bassal amesema shambulizi hilo lilitokea katika shule ya Fahmi Al-Jar-jawi. Ameongeza kuwa wengi wa waliojeruhiwa ni wanawake na watoto.
Hata hivyo jeshi la Israel limesema eneo hilo lilikuwa linawahifadhi magaidi waliokuwa wakishirikiana na kundi la Hamas.
Mkuu wa shirika la misaada kwa Gaza ajiuzulu
Wakati Israel ikiimarisha mashambulizi yake ya kulisambaratisha kundi la wanamgambo wa Hamas, viongozi wa dunia wanaokutana uhispania watoa wito wa usitishwaji vita, makundi ya kutoa misaada ya kitu yakisema misaada inayotolewa haitoshi kuwafikia watu wa Gaza wanaokumbwa na njaa na changamoto za kiafya.