MigogoroMashariki ya Kati
Watu 9 wauwawa kwa shambulio la Israel Ukanda wa Gaza
15 Machi 2025Matangazo
Msemaji wa Shirika hilo Mahmoud Bassal amesema wafanyakazi kadhaa wa shirika la hisani la Al Khair pia wameuwawa katika shambulio hilo la droni lililolilenga gari lao.
Jeshi la Israel wakati lilipojibu kuhusu baadhi ya matukio yaliyoripotiwa na mamlaka za Gaza limesema vikosi vyake vimeingilia kati na kutibua vitisho vya waliowaita "magaidi" waliokuwa wakivikaribia na kutega mabomu chini ya ardhi.
Soma zaidi: Israel yatakiwa kutekeleza hatua za kusitisha mapigano Gaza
Kundi la Hamas limesema shambulio hilo ni ukiukaji wa wazi ya makubaliano ya kusitisha vita. Maafisa wa afya wa ukanda huo wanasema makumi ya watu wameuawa tangu makubaliano hayo yaliposainiwa.