Serikali ya Sudan yaishutumu UAE kwa "uchokozi"
7 Mei 2025Matangazo
Miripuko ilisikika mjini, ingawa haikubainika mara moja iwapo ilikuwa karibu na kambi ya kijeshi ya Flamingo.
Port Sudan imekuwa ikikabiliwa na mashambulizi kwa siku kadhaa - ikiwa ni pamoja na mashambulio ya ndege zisizo na rubani yaliyoripotiwa na vikosi vya waasi wa RSF- ambavyo pia vimeteketeza bohari kubwa zaidi ya mafuta nchini humo na kuharibu lango kuu la misaada ya kibinadamu.
Soma pia: Kambi ya jeshi la anga la Sudan yashambuliwa kwa droni
Huku haya yakiarifiwa, serikali inayoongozwa na jeshi ya Sudan imetangaza kusitisha uhusiano wa kidiplomasia na Umoja wa Falme za Kiarabu, ikilishutumu taifa hilo la Ghuba kwamba linawapa silaha waasi wa RSF.