UchumiEthiopia
Serikali ya Ethiopia yaidhinisha ongezeko la bajeti yake
7 Juni 2025Matangazo
Ofisi ya Waziri Mkuu wa Abiy Ahmed imesema kuwa Bajeti hiyo itasaidia katika kuhakikisha usalama wa kitaifa, kuongeza uzalishaji na kusaidia watu walioathirika na majanga.
Taifa hilo la Afrika Mashariki, ambalo lilisaini makubaliano ya miaka minne na Shirika la Fedha Ulimwenguni (IMF), liko katikati ya mageuzi makubwa yakiuchumi, yakiwemo kulegeza thamani ya sarafu ya birr na juhudi za kurekebisha madeni yake.
Wiki iliyopita, Ethiopia na IMF walifikia makubaliano ya awali ya mkopo wa dola bilioni 3.4 kutoka kwa shirika hilo la fedha.