Rwanda yavunja uhusiano wa kidiplomasia na Ubelgiji
17 Machi 2025Matangazo
Wakati huohuo, Ubelgiji nayo imetangaza kuwafurusha wanadiplomasia wa Rwanda huku waziri wa mambo ya nje wa nchi hiyo Maxime Prevot akitaja kusikitishwa na uamuzi huo wa Rwanda akisema hauna uwiano na inaonyesha kuwa nchi hiyo haipendelei kushiriki kwenye mazungumzo.
Soma pia:Waasi wa M23 wanavyojinufaisha na madini ya Kongo
Hayo yanajiri wakati hapo jana, rais Paul Kagame wa Rwanda aliituhumu Ubelgiji kwa kuichonganisha Rwanda na mataifa mengine ili iwekewe vikwazo kutokana na mzozo huo. Leo, mataifa ya Ulaya yamewawekea vikwazo makamanda kadhaa wa kijeshi wa Rwanda na Kongo.