Rwanda yazungumza na Marekani kuhusu kupokea wahamiaji
5 Mei 2025Matangazo
Waziri huyo wa mambo ya nje wa Rwanda, Olivier Nduhungirehe, ameyasema hayo alipohojiwa Jumapili, kwenye kituo cha televisheni ya taifa ambapo aliweka wazi kwamba mazungumzo yanafanyika pamoja na Marekani kuhusu hatua hiyo, japo bado hayajafikia hatua ya kuzungumzia yamefikia wapi na mwelekeo wake ukoje.Soma pia: Mpango wa kuwapeleka waomba hifadhi Rwanda umekosolewa na wengi
Katika miaka ya hivi karibuni Rwanda imejiweka katika nafasi ya kuwa kituo cha kuwapokea wahamiaji wasiotakiwa kwenye nchi za Magharibi.
Mwaka 2022 ilisaini mkataba wa kupokea maelfu ya waomba hifadhi kutoka Uingereza,mkataba ambao ulifutwa mwaka jana na waziri mkuu Keir Starmer baada ya kuingia madarakani.