Rutte: NATO kuongeza kwa kiasi kikubwa uwezo wa ulinzi
4 Juni 2025Matangazo
Rutte amesema malengo hayo yanaweka wazi kiwango cha misaada ambacho washirika wanahitaji kutoa ili kuimarisha ulinzi wao.
Pia amesema kuwa ulinzi wa anga na makombora, silaha za masafa marefu na mipangilio, ni miongoni mwa masuala yao ya kipaombele.
Ujerumani yatafuta kuungwa mkono Ulaya bajeti ongezeko la ya ulinzi
Katibu huyo ameongeza kuwa wanahitaji raslimali zaidi, vikosi na uwezo ili kuwa tayari kukabiliana na tishio lolote, pamoja na kutekeleza kikamilifu mipango ya pamoja ya ulinzi.
Mawaziri wa ulinzi wa NATOwatakaokutana Brussels kesho Alhamisi, wanatarajiwa kupitisha rasmi mipango mikuu ya siri.