NATO yaridhia ongezeko la asilimia 5 katika bajeti yake
26 Juni 2025Matangazo
Rutte amesema hatua iliyochukuliwa ni ya ghafla lakini muhimu katika kuimarisha ulinzi wa pamoja.
Akizungumza na waandishi habari mjini The Hague katibu huyo wa NATO amesema makubaliano hayo yanayotarajiwa kufikiwa ifikapo mwaka 2035 yataifanya Jumuiya kuwa imara zaidi.
NATO: Wanachama sa kuongeza michango yao kwa asilimia 5
Kando na hayo Rutte pia alisisitiza uungwaji mkono wa jumuiya hiyo usiotetereka kwa Ukraine akisema ni lazima Rais Volodymyr Zelensky aendelee kusaidiwa kijeshi ili aweze kukabiliana na kitisho cha usalama kutoka Urusi.
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky anatarajiwa kukutana na rais Trump pembezoni mwa mkutano huo. Ujerumani imesema inajaribu kumshawishi Trump kuipa kipaumbele nchi ya Ukraine.