Ruto akosoa wapinzani kabla ya maandamano ya GenZ
22 Juni 2025Matangazo
Waharakati na familia za waliopoteza maisha katika maandamano hayo wameahidi kufanya maandamano mapya Juni 25 kama kumbukumbu, wakiwataka polisi na wanasiasa kuruhusu yafanyike kwa amani.
Akizungumza katika kaunti ya Meru jana Jumamosi Ruto amesewakosoa wapinzani wake kwa kusema kuwa wanatumia kauli za ubinafsi na propaganda dhidi ya uongozi wake.
Maandamano ya mwaka jana yaliibua mgogoro mkubwa wa uongozi wa serikali ya Ruto, na kuilazimu kusitisha kwa kiasi ongezeko la kodi na kutangaza mabadiliko katika baraza la mawaziri.
Wiki iliyopita maandamano mengine yaliibuka katika taifa hilo la Afrika Mashariki kupinga ukandamizaji wa polisi.