Rubio; Makubaliano ya Urusi na Ukraine yapatikane haraka
27 Aprili 2025Matangazo
Rubio ameliambia shirika la habari la NBC katika kipindi kinachojulikana kama ''Meet the Press'' kwamba Washington haiwezi kuendelea kutumia muda wao na raslimali kwa juhudi hizo ikiwa hakutakuwa na ufanisi.
Rais Trump akutana na Zelensky na kufanya mazungumzo
Ameongeza kusema kuwa wiki iliyopita ilikuwa ya kujaribu kutafakari ukaribu wa pande hizo na ikiwa ukaribu huo unastahili kutumika kwa Marekani kama mpatanishi.
Hata hivyo Waziri huyo wa mambo ya nje wa Marekani hakuweka wazi muda maalum ambao utawala waTrump uko tayari kusubiri kupata mafanikio.